Kutokana na kukamatwa kwa mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi leo mjini Dodoma huu ndo ukweli kutoka Dodoma….
"kuhusu Joseph Mbilinyi 'Sugu',
Mbunge wa Mbeya Mjini. Ni kweli alikuwa polisi Dodoma, alikoitwa kwa
madai ya kutoa lugha ya matusi kwa Ndugu Mizengo Pinda, lakini
hajaandikisha maelezo, kwa sababu 3, zifuatazo:
1. Wakili wake, Tundu Lissu, amewaambia kuwa Polisi hawawezi kumkamata
na kumhoji Mbunge Sugu, iwe ukumbini, maeneo ya bunge, au nje ya maeneo
ya bunge, wakati bunge likiendelea, kutokana na parliamentary immunity
aliyonayo hadi polisi watakapofuata taratibu zinazotakiwa.
2. Neno hilo wanalotuhumu kuwa ni lugha ya matusi, si tusi kwa sheria
za nchi yetu, bali linaweza kutumika kwa vitu au mtu anayefanya matendo
au kusema maneno yanayostahili kuitwa hivyo.
3. Wakili wake (Tundu Lissu)kawauliza, nani mlalamikaji katika tuhuma
hizo, je wamepokea malalamiko ya Ndugu Pinda mwenyewe? Majibu yalikuwa
ya kigugumizi"
Wameondoka polisi kwa makubaliano ya kurudi kesho asubuhi.
No comments:
Post a Comment