Wakazi wa
mji muhimu wa Sudan ambao ulishambuliwa na wapiganaji hapo jana, wamechoma moto
majengo ya serikali na kuwarushia mawe wakuu wa jimbo.
Walikuwa wakipinga ziara ya gavana wa jimbo ambaye
alizuru mji wa Umm Rawaba, kwenda kuona uharibifu uliosababishwa na mapigano.
Wapiganaji wa kundi la JEM na wapiganaji wengine
waliuteka mji wa Umm Rawaba kabla haujakombolewa na jeshi la serikali.
Kawaida wapiganaji wa GEM wanaendesha harakati zao
katika jimbo la Darfur.
Waandishi wa habari wanasema shambulio hilo
lilikuwa la kijasiri kwa sababu limetokea katika jimbo la Kordofan Kaskazini,
eneo ambalo lilikuwa halikuathirika na harakati za wapiganaji.
<
No comments:
Post a Comment