WADAU WA ELIMU KIBAHA
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12 February, 2013/14:40:45
Masuala ya ruzuku na kukosekana kwa walimu wa kike wa kutosha katika
maeneo ya pembezoni kumezua mjadala wa kadiri katika kikao cha wadau wa
elimu katika halmashauri ya wilaya Kibaha, chenye lengo la kung'amua
mafanikio na mapungufu katika suala zima la usimamizi wa elimu.
Mmoja wa wajumbe waliohudhuria kikao hicho kutoka katika Kata ya
Magindu amelalamikia idara ya elimu kwa kuzorotesha upelekaji wa ruzuku
ya dola kumi kwa kila mwanafunzi na hivyo kuathiri uboreshaji wa elimu,
amefafanua upatikanji wa fedha hizo umekuwa na mizengwe mingi na hata
zikipatkana zinakuwa zimeshachelewa.
Mjumbe huyo ameitaka
serikali kuhakikisha inafikisha fedha za ruzuku kwa wakati na wachukulie
suala hilo kama wajibu na sio hisani kama watendaji wengi
wanavyolichukulia na kusaidia kuwaepusha baadhi ya watendaji kujikuta
wanatoa fedha za mifukoni mwao kuendesha shughuli za shule.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya shule ya msingi MUYUMBO, BW. MORETO MORETO
amebainisha tatizo la walimu wa kike katika shule yao, jambo ambalo
linawapa wakati mgumu wanafunzi wa kike wanapopatwa na matatizo
yanayosabishwa na maumbile yao.
Hivyo ameitaka idara ya elimu
kuwa na utamaduni wa kutembelea shule hiyo mara kwa mara kwani kuna
uchakavu mkubwa wa majengo na samani za shule, tatizo ambalo
linachangiwa na kutokuwepo kwa wakaguzi wa kupitia shule na kuziangalia
maendeleo yake kama ilivyokuwa zamani.
Afisa elimu msingi
halmashauri ya wilaya ya Kibaha BIBI. WINFRIDA MBUYA akijibu hoja za
wajumbe hao wawili amesema suala la ruzuku kwa shule za msingi hilo ni
tatizo la Hazina ambapo yeye kwa nafasi yake hawezi kulisemea kutokana
na taarifa ya kutokuwepo kwa fedha za kutosha kukidhi mahitaji
yanayohusiana na idara yake, na kuhusiana na suala la shule ya msingi ya
Muyombo yeye kasema huwa wanaitembelea.
No comments:
Post a Comment