Taarifa za uhakika zilizonifikia kama saa moja hivi iliyopita zinaeleza
kwamba mapigano yameibuka na yanaendelea kati ya Wakristo na Waislamu
katika mji Mdogo wa Buselesele wilayani Chato Mkoani Geita wakigombania
kuchinja.
Ni kwamba jana wakristo alitangaza kwenye mkutano wa hadhara kwamba leo
jumatatu wanaanza kuchinja na kuuza nyama kwenye bucha zao,na
wakaitangaza moja ya bucha zilizoko katikati ya soko la Mji wa Katoro
kwamba ndilo litakuwa likiuza nyama za wakristo.
Ilipofika asubuhi ya leo majira ya saa 9 waislamu wakapata taarifa
kwamba bucha hiyo inauza nyama kwa ajili ya wakristo,huku bucha zao
zikionekana kudorora ambapo waliamua kwenda na kuanzisha vurugu kwenye
bucha hiyo.
Kwa mujibu wa Taarifa hizo tayari aidi ya watu 10 wamejeruhiwa kwa
kukatwa mapanga ambapo mmoja hali yake inaelzwa kuwa mbaya na
amekimbizwa ktika hospitali ya wilaya ya geita,tayari polisi wa kikosi
maalum cha kutuliza ghasia FFU kikiongozwa na Mkuu wa upelelezi wa
makosa ya jinai mkoani Geita wamewasili eneo la tukio.
Nitaendelea kuwajuza kinachoendelea kadri nitakavyokuwa Napata tarifa
ikiwa ni pamoja na picha za majeruhi.Kwa wale wenyeji wa eneo hilo ni
vigumu kutofautisha mji wa Katoro wilayani Geita na Buselesele wilayani
chato kwa sababu ni miji iliyoko kwenye eneo moja na inaingiliana kwa
kila kitu.
No comments:
Post a Comment