CHADEMA YAENDELEA KUTESA KIBAHA
Ben Komba/Pwani-Tanzania/10-Feb-13/13:42:54
Chama cha demokrasia na maendeleo kimewataka wananchi kutokubali
kurubuniwa kwa kuwaambia CHADEMA ni chama cha kidini kunakosababishwa
kwa baadhi ya vyama kutumia propaganda hiyo kutaka kuwagawa watanzania
na baadaye kuwatawala kwa kufuata mifumo ya kurithishana kama
inavyojidhihirisha hivi sasa.
Akiongea katika mkutano wa vuguvugu la mabadiliko inayoendelea nchi hivi
sasakatika viwanja vya stendi ya Mzenga katika mamlaka ya mji mdogo wa
Mlandizi yenye kulenga kutekeleza kauli ya mwaka wa nguvu ya umma
inayoeendeshwa na chama cha demokrasia na kufanikiwa kuleta mitazamo
chanya kwa wakazi wa wilaya ya Kibaha kutokana na kuwepo piga nikupige
ya mikutano kati ya chama cha CHADEMA na CCM.
Kada wa chama
cha demokrasia na maendeleo kutoka Arusha, BW.ALLY BANANGA amesema cha
cha CCM kimekuwa chama cha kurithisha uongozi na kuyatupa kando malengo
ya awali ya uanzishaji wa chama hicho ambayo yalikuwa hayana lengo la
kujenga himaya za kisultani kwa baadhi ya viongozi na familia zao kama
ilivyo hivi sasa kwa kuzusha mambo ambayo hayana ukweli wowote katika
kujaribu kuwagawa watanzania kiimani.
BW. BANANGA amebainisha
kumekuwepo na harakati kubwa katika kuhakikisha wanafanikiwa kukamata
dola mwaka 2015 na kuwaasa wana Kibaha ambo wamechoka kunyanyaswa na
kukandamizwa na chama tawala kuunga mkono harakati hizo za CHADEMA zenye
lengo la kumkomboa mtanzania na mgogoro mkubwa wa kimfumo
tunaokabiliana nao kutokana na baadhi ya watu kujiona kama wana hati
miliki na Taifa hili.
No comments:
Post a Comment