Wednesday, December 7, 2011

Wafanyasiasa: Wametushindwa Mtaani Wametufata Online by Tanganyikan

Siku za karibuni Watanzania tulipopo katika tovuti jamii tumeshuhudia kitu ambacho nakiita “Series”. Kwa bahati mbaya imenichukua muda kuishtukia series yenyewe kwa hiyo ni ngumu sana kusema tuko season ya ngapi na episode gani.
Picha lenyewe lilianzia Jamii Forums ambako kambi za wanasiasa wambao wanaoneakana wamejiandaa kuichukua nchi katika uchaguzi mkuu 2015 zilianza kujionyesha wazi wazi moja ikiwa ni ya waziri mkuu alietema mzigo awamu ya kwanza Edward Lowassa na nyingine ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Edward Membe. Kwa upande wa JF hizi kambi hazijifichi, tunawajua kina nani ni mashabiki wa nani na kina nani wanampinga nani. JF sina tatizo kwa sababu kusema kweli kule ndio Social Network ambayo kila kichwa ambacho kinajua siasa kipo na ndio maana ikaitwa The Home Of Great Thinkers.
Kitu kinachonikera ni kitendo cha hawa wataka madaraka kuvamia sehemu ambazo Watanzatulikuwa tumekaa kwa amani bila kuleteana stress na kuchoshana, Faceboook na Twitter. Na style waliyoingia nayo ni ile ya kuchafuana. Tulianza na Mkurugenzi wa Habari Ikulu ndugu Salva Rweyemamu, account yake ikawa hacked na mtu asiejulikana wakati huo Rais Kikwete alikuwa anajiandaa kwenda kwenye safari yake ya Australia. Aliehack akaanza kuweka madude ya ajabu na akafollow watu kibao twitter, kila mtu alijua kabisa kuwa Salva kawa hacked kwa hiyo hakuna aliejali sana. Kinachonishangaza ni kitendo cha Salva Rweyemamu mwenyewe kutokanusha kwenye vyombo vya habari kama vya serikali ambayo yeye ndo kama msemaji na pia mpika propaganda zote zinazotoka mle ndani ya Ikulu kwenda Magazeti yanayomilikiwa na serikali. Ameacha tu jamaa anaendelea kupeta.
Haya, Wakati picha la Salva linaanza kupoteza mvuto mara kaibuka Mama.. aliingia mama First Lady kupitia account yake ambayo ilikuwa inatumika toka wakati wakati wa Kampeni za uchaguzi 2010 mara ghafla bin vuu tukaona anaanza “kum-snitch” mumewe tena ikiwa ni ile wiki ya Mheshimiwa Kikwete kukutana na CHADEMA ikulu kuhusu majadiliano ya sheria mpya ya uundwaji wa Katiba. Sihitaji kusimulia kilichotokea kwenye account ya Bi Mkubwa unaweza kusoma Timeline yake kwa kubofya hapa.
Mara wakati tunaanza kupiga miluzi na kuanza kuona Mama hana jipya, siku ya Jumanne Desemba 6 parapanda likalia, mtu tulieamini kwamba kwa sasa yuko kwenye bohari la kusubiria siku ya hukumu ili tujue kama unaenda Ahera au Kuzimu sio mwingine bali Gavana wa Benki Kuu ambaye alitupiwa  kila zigo la misumari ya madudu yaliyofanyika kwenye kashfa za ufujaji wa hela za wananchi katika Benki Kuu Tanzania “BOT” ndugu Daudi Balali  nae akaibuka twitter na jina lake lile lile la Daudi Balali. Huyu jamaa nimekuja kushtukia kuwa ananifollow kama saa moja jioni na kabla ya hapo niliangalia followers wangu wapya saa sita alasiri ikimaanisha ndani ya hayo masaa matano baada ya mimi kuangalia jamaa alifungua account akaanza kufollow watu na kwa namna twitter kule mbinguni/motoni ilivyo fasta ndani ya hayo masaa machache kafollow watanzania kibao. Anachodai jamaa mwenyewe anasema yeye hajafa na yuko visiwa flani anakula raha na kashasema kuwa ana siri za kutuambia kuhusu kifo chake ambazo kiujumla lazima ziwataje Wanasiasa wa Tanzania.

Kitu tunachotakiwa kujiuliza ni je kwa nini hawa watu wanaofanya huu upuuzi wa kuibiana password wanaonekana kuwa na kasi ya ajabu na hakuna mtu au kiongozi yeyote serikalini au wizara husika anaeonekana kujali kuhusu hili suala la majina ya Watu walioko ndani ya Utawala wa Rais Kikwete kutumiwa vibaya kwenye mitandao ya kijamii? Tuliona Wizara ya Mambo ya ndani ilivyoshadadia ule waraka uliowekwa Jamii Forum na baadae kusambazwa kwenye email kwa watu mbalimbali kuhusu Kikosi kilichotoa onyo kuwa kinataka kumpindua Rais Kikwete. Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha waziri wa Mambo ya Ndani alitupiga mikwara kuwa yeyote atakae-forward hiyo email atachukuliwa hatua za kisheria na tukaogopa ule waraka umekufa bila kelele. Sasa ni kwa nini hatua hiyo hiyo haijachukuliwa kwa mtu anaeendeleza huo mchezo twitter na facebook ameachiwa aweke kitu anachokitaka?
Kinachoonekana hapa ni kuwa hawa wanasiasa sasa wameamua kutuvamia kwenye social media, staili waliyoingia nayo ndio bado sijajua ni kambi ya nani inahusika. Wamegundua kwamba sasa hivi watu tunapenda kujadili mambo yanayotokea kwenye ulingo wa siasa kwa kuongea ukweli bila kumuogopa mtu na tumekuwa tukiikosoa wazi wazi serikali pale inapokosea.
Na bila kujijua tumeukwaa mtego wao, wanapoanza kuongea mambo yao tunawashabikia mimi nikiwa mmoja wapo ambao nilimshangilia bi mkubwa alipoanza kumnanga wazi mumewe. Kitu tunachotakiwa kujua ni kuwa hawa watu wamekuja na mkakati mpya, wanajua wazi kuwa wanao uwezo mkubwa wa kutawala vyombo vya Habari vya ndani kama Magazeti na Redio. Tunaona wenyewe namna magazeti siku hizi yalivyojaa ushabiki wa vyama. Kuonyesha namna walivyopania kutukukamata wamepiga hatua kubwa zaidi kwa kununua baadhi ya wamiliki wa blog, hili najua kila mtu analifaham. Kuna bloggers ambao miaka michache iliyopita walikuwa mstari wa mbele kutetea haki za Wananchi lakini sasa hivi hatunao ghafla wamekuwa mazezeta na wanasema hewala kwa kila kitu kinachotokea serikalini ingawa mwisho wa siku wanaaibika. Kitu kilichowashinda mpaka sasa ni namna ya kuwanunua watu kama Udadisi, Chahali, Maria Sarungi, Michael Dalali, Yericko Nyerere, Issa Mwamba, Mshaba, Irenei, Semkae, iAlen,tsavonglah, omarilyas, Nanyaro Patrick na wengine wengi sijawataja ambao wamekuwa na fikra zisizoyumbishwa na matukio yao wanayoyatengeneza ili kutuvuruga. Wanajua hawawezi kuweka ofa mezani ya kutunyamanzisha wote kwa pamoja, wanajua hizi website ni za mzungu na hawana uwezo wa kutuchagulia tuongee nini na kwa wakati gani kwa hiyo wameamua kutuundia mkakati wa kuhakikisha kinatokea kile ambacho wazungu wanaita “divide and rule”.
Tunatakiwa kujua kitu kimoja, hawa watu wanaofanya huu mchezo wapo kati yetu, ni marafiki zetu ambao inawezekana hata tunapokuwa tunajadili siasa na wao ni wachangiaji wazuri tu ila wanajifanya anti-government. Tatizo ni kwamba hatuwafahamu kwa majina, wanarusha ngumi gizani alaf wanasikilizia nani atatoa mguno wa maumivu. Kama kweli tunataka uwepo wetu mtandaoni usionekane kuwa ni wa kihuni tujitahidi sana kuwapotezea hawa watu. Unapozidi kumsemesha mtu kama balali inamaanisha sio kwamba wewe tu ndio utakuwa unajibizana nae, kumbuka kuna followers wako ambao wanakuwa wanafatilia mnachoongea na kuweka RT kwa hiyo inasambaa kwa familia ya Watanzania wote mtandaoni. Kama kweli tunataka kukomesha hii tabia ya kutufanya mabwege na mazezeta kwa kutuchagulia habari gani tuisikie tunatakiwa tuwapotezee, wakiongea kaa kimya wala usipoteze muda kuongea nao. Usitegemee kuwa huyo anaejiita balali au mama salma atakuja na jipya zaidi ya propaganda ambazo mwisho wa siku ni za kumfanya mtu fulani apate kura 2015. Njia wanayoitumia hapa ni kuongea kitu ambacho wanajua Watanzania wengi wanakijadili kila siku, serikali. Wamekuwa mstari wa mbele kuikosoa serikali. Kabla hujashabikia tambua kwamba hawa sio wenzetu. Wakati wewe unaikosoa serikali kwa kufikiria vizazi vijavyo wao wamelenga kura yako na uchaguzi mkuu ujao 2015.
Tambua kitu kimoja, Wapo kati yetu.  Daktari Jakaya aliseka “Za kuambiwa Changanya na Zako”
Ni Hayo tu.

No comments:

Post a Comment