Wednesday, December 25, 2013

TAKWIMU ZA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI


Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/26/2013 9:41:12 AM
Takwimu za Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani zimebainisha kuwa katika kipindi cha mwaka 2013, jumla ya matukio 3705 yameripotiwa katika vituo mbalimbali vya Polisi, kati ya makosa hayo ni Mauaji, Kubaka, Kulawiti, Wizi wa watoto na utupaji wa watoto.

Akisoma taarifa ya utekelezaji ya Jeshi hilo katika mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi mwandamizi, URLICH MATEI amebainisha kuwa makosa hayo yamegawiwa katika makundi manne, makosa dhidi ya ubinadamu, makosa dhidi ya kuwania mali, Makosa dhidi ya maadili ya jamii na makosa ya usalama barabarani.

Kamanda MATEI amezungumzia upande wa makosa ya kuwania mali ambayo yametokea katika kipindi cha mwaka 2013 ni pamoja na kukamatwa kwa noti bandia zenye thamani ya milioni 3,040,000/= huko Chalinze katika wilaya ya Bagamoyo ambazo zilikuwa zimehifadhiwa ndani ya bahasha.

Kwa upande wa uhalifu dhidi ya maadili ya jamii, Kamanda MATEI ameongeza kuiwa Jeshi la Polisi limeweza kudhibiti maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani kwa kufanya misako na kufanikiwa kukamata wahamiaji haramu kutoka ETHIOPIA na Somalia.

Aidha katika kipindi hicho wilayani Kisarawe katika eneo la Kauzeni kata ya Vikumburu , Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukamata vipande 70 vya meno ya Tembo kwenye kizuizi cha ukaguzi wa mazao ya misitu na kuwakamata watuhumiwa 9 kati yao 2 wakiwa askari wa Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi mwandamizi ULRICH MATEI amewaasa madereva kuwa makini wanapoendesha magari katika kipindi hiki cha sikukuu kutokana na kuwepo kwa shamrashamra zinazoambatana nazo.

No comments:

Post a Comment