Ben Komba/Pwani-Tanzania/Thursday, July 18, 2013
Mkuu wa wilaya ya Kibaha BI.HALIMA KIHEMBA amewataka wakazi
ambao wanasemekana kuvamia eneo la BW. MOHAMED SUMA kuondoka mara moja ili
kutoa fursa kwa mmiliki kuliendeleza.
Akiongea na wakazi wa Mtakuja katika kata ya Pangani
halmashauri ya mji wa Kibaha BI.KIHEMBA ambaye ameshafika katika eneo hilo mara
tatu katika suala zima la kujaribu kutafuta suluhu kati ya mmiliki na wakazi
ambao wanasemekana wamevamia.
BI.KIHEMBA akisoma barua iliyotoka kwa kwa mmiliki wa shamba
hilo, BW.MOHAMED SUMA ambayo imefafanua kuhusiana na watu ambao yeye
amewakabidhi eneo la heka 16 kwa watu wanane kila mmoja heka 2.
Kwa hatua hiyo BI.KIHEMBA amewasihi wakazi hao kuondoka
katika eneo hilo toka wanaokaa eneo hilo wanadai wamepewa bure hivyo amewataka
nao kurudisha eneo hillo bure ili kuondoa usumbufu kwa ofisi yake.
Naye aliyekuwa Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mtakuja BW.
LONGINO KASONTA amesema mzigo mkubwa anasukumiziwa yeye ilihali ambay
amesababisha mtafaruku huo aliyekuwa mtendaji kata ya Pangani, BW.JAMES NOYA
akiwa haguswi kabisa.
BW.KASONTA amebainisha kuwa mmiliki wa eneo hilo lenye heka
108, aliridhia binafsi kuto heka 16 kwa baadhi ya wananchi, Lakini bila kutoza
fedha zozote, mambo yakabadilika mara baada ya mtendaji wa Kata kuhamishiwa
hapo ambapo alianza kugawa eneo hilo kwa ada ya sh.20,000/=, kitu ambacho
kilikuwa kinyume na matakwa ya mmiliki.
No comments:
Post a Comment