USHAURI WA MBUNGE KOKA WA KIBAHA
Ben Komba/Pwani-Tanzania/09:46/09/07/2013.
Wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa nchini wameshauriwa kuwa na
utamaduni wa kusaidia taasisi mbalimbali za kijamii katika suala zima la
kuaharakisha maendeleo ya nchi na wananchi wenyewe.
Hayo
yamezungumzwa na mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini, BW.SYLVESTER KOKA
wakati akikabidhi msaada wa madawati 50 kwa shule za msingi Jitihada na
Lulanzi yaliyotolewa na taasisi ya mikopo kwa wafanyakazi wa umma
FAIDIKA.
BW.KOKA amesema kwa
jinsi anavyofahamu uwepo wa wafanyabiashara wenye fedha nyingi ambao
wangefuata nyayo za Taasisi ya FAIDIKA wangeweza kusukuma mbele gurudumu
la maendeleo.
Amebainisha kwa sasa nchi yetu ina
wafanyabiashara mbalimbali wakubwa ambao kama wangekuwa wanatoa asilimia
hata 5 ya walicho nacho katika kuchangia shughuli za kijamii basa kero
nyingi za kijamii zingepungua hususan upande wa elimu.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa taasisi ya mikopo ya FAIDIKA, BW.HARUN FERUZ
amesema taasisi yake imekuwa na utamaduni wa kuchangia madawati katika
maeneo mbali yenye uhitaji ili kuweza kupunguza kero hiyo.
BW.
FERUZI ameongeza kuwa kabla ya kutoa madawati hayo, wanafanya utafiti
katika shule husika kubaini mahitaji halisi ya madawati na wamekuwa
wakitoa kwa kadri ya uwezo wao kutokana na ukosefu wa madawati mashuleni
kuwa mgumu.
Akishukuru kwa kupokea madawati hayo Mwalimu mkuu wa
shule ya msingi Lulanzi aliishukuru Taasisi ya mikopo ya FAIDIKA kwa
kuweza kutoa mchango huo na kuwataka wafadhili wengine kujitokeza
kusaidia shule zenye ukosefu mkubwa wa madawati.
No comments:
Post a Comment