Thursday, January 31, 2013

MBUNGE WA ARUSHA MJINI AUNGURUMA

" Ninatoa Mwezi mmoja tu nataka Halmashauri ya Jiji la Arusha iwe safi na hii kazi Mkurugenzi anapaswa kuifanya kwa haraka sana na sioni na siko tiyari kupewa sababu yeyote ile ya kwa nini Arusha ni Chafu.

Na baada ya mwezi mmoja Mimi Mbunge nitaanza kukusanya takataka mjini na kumpelekea Mkurugenzi ofisini kwake ili kama Hazioni wananchi wamsaidie kuziona na ninaomba Wananchi wote nitakapotangaza tarehe hiyo mjitokeze kwa wingi ili tuwasaidie Jiji kukusanya Takataka na kumwaga mbele ya ofisi zao ili wajue kwa uhalisia kero ya uchafu Mjini .

Sasa kazi ni kwa vitendo na hakika najua Serikali ni lazima iwajibike kwa watu wa Arusha .

No comments:

Post a Comment