TAARIFA KUTOKA KASKAZINI MWA MALI
ZINAELEZA KUWA WAPIGANAJI WA KIISLAMU WAMEVUNJA MAKABURI KADHA YA KALE KATIKA
MJI WA TIMBUKTU.
KIONGOZI MMOJA WA WAPIGANAJI HAO
AMELIAMBIA SHIRIKA LA HABARI LA UFARANSA KWAMBA MAKABURI YOTE MJINI TIMBUKTU
YATAVUNJWA, KWA SABABU YANAKWENDA KINYUME NA UISLAMU.
KATI YA MWAKA HUU MAKABURI KADHA
YALIVUNJWA KATIKA MJI HUO AMBAO NI ENEO LA KUHIFADHIWA KUFUATANA NA UMOJA WA
MATAIFA.
MAKUNDI YA WAPIGANAJI WA KIISLAMU NA
MENGINEYO YALITEKA ENEO LA KASKAZINI LA MALI BAADA YA SERIKALI YA TAIFA
KUPINDULIWA AWALI MWAKA HUU.
SIKU YA ALKHAMISI UMOJA WA MATAIFA
ULIPITISHA AZIMIO KUKUBALI KIKOSI CHA NCHI ZA AFRIKA KUTUMWA MALI.
No comments:
Post a Comment