Thursday, September 20, 2012

UCHAGUZI BUBUBU


Chama cha wananchi CUF kinajiandaa kwenda mahakamani kupinga ushindi wa mgombea wa CCM Hussein Ibrahim Makungu katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Bububu uliofanyika Jumapili iliyopita.

Akizungumza na Zenji FM radio, mkuregenzi wa mawasiliano na haki za binadamu wa CUF Salim Bimani amesema wanasheria wa chama hicho wanaandaa taratibu za kisheria ili kufungua kesi hiyo.

Amesema wana ushahidi wa kutosha wa kukiukwa taratibu za uchaguzi ikiwemo upandikizaji wa wapiga kura.

Bimani amesema taratibu za kisheria za kufungua madai hayo zinatarajiwa kukamilika ndani ya siku 14 tokea kutangazwa mshindi huyo.

Chama cha wananchi CUF kimepinga matokeo ya uchaguzi yaliompa ushindi mgombea wa CCM Makungu kwa kupata asilimi 50.7 ya kura dhidi ya mgombea wa CUF Issa Khamis Issa aliepata asilimia 48.2 ya kura.

Wakati huo huo mbunge wa jimbo la Mtoni Faki Haji Makame amekanusha taarifa za kukamatwa na jeshi la polisi na kufikishwa mahakamani akidaiwa kupigana hadharani siku ya uchaguzi huo.

Akizungumza na wandishi wa habari huko afisi ya wilaya CUF Vuga amesema taarifa hizo alizonukuliwa kamishna wa polisi Zanzibar zina lengo la kupotosha ushahidi dhidi ya kadhia ya kupigwa iliyomkuta siku hiyo.

Makame amesema siku ya tukio hilo alipigwa na vijana watatu kati yao wawili walikamatwa na jeshi la polisi kituo cha Bububu, lakina anashangazwa bado hawajafunguliwa mashtaka

No comments:

Post a Comment