Klabu ya Ligi kuu ya England, Chelsea ni kwamba klabu hio imeachana na kocha Andre Villas-Boas leo jumapili.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 34 amepoteza
kazi hio saa 24 baada ya kupoteza jana pambano la Ligi dhidi ya klabu ya
West Bromwich Albion 1-0.Tangazo la Chelsea limesema kua aliyekua naibu wa Kocha huyo Roberto Di Matteo atashikilia wadhifa wa Kocha hadi mwisho wa msimu.
Kocha huyo inasemekana alijenga uhasama baina yake na wachezaji wakuu katika klabu ya Chelsea, akiwemo kiungo Frank Lampard na vilevile mfululizo wa matokeo mabovu akiweza tu ushindi mara moja katika mechi saba.
Matokeo haya hasa ndio yaliyosababisha mmiliki wa klabu ya Chelsea, Roman Abramovich kumchukulia hatua.
Msumari wa mwisho ulitokea jumamosi baada ya Chelsea kupoteza mechi dhidi ya klabu ya West Bromwich Albion 1-0 kupitia Garth McAuley.
Taarifa ya bodi ya Chelsea iliyotangaza kuvunjika kwa ndoa kati ya Chelsea na Villas Boas, imesifu juhudi zake na kusikitika kua hawakuweza kudumu zaidi ya hapa kutokana na matokeo mabovu na kukosekana kwa dalili kua hali hio inaweza kubadilika.
Villas Boas aliletwa Chelsea kubadili kikosi kichovu baada ya ushindi wake wa vikombe vinne akiwa na klabu ya Porto msimu uliopita, lakini mda wake na Chelsea uligubikwa na habari za mvutano kama ulioarifiwa na Ma meneja waliomtangulia kua ndio uliosababisha kushindwa kuiongoza Chelsea na hivyo kutimuliwa.
No comments:
Post a Comment