Watu zaidi ya 800 bado wametoweka nchini Philippines baada ya kimbunga
kilichosomba vijiji kusini mwa nchi, katika kisiwa cha Mindanao.
Maelfu ya wanajeshi wanashiriki katika shughuli za uokozi, na bado
wameshindwa kufikia vijiji vya mbali ambavyo vimefunikwa na mafuriko na
maji ya pwani yaliyojaa.
Imethibitishwa kuwa watu zaidi ya 650 wamekufa.
Wakuu wamelaumiwa kwa kutowaonya watu mapema, kwamba dhoruba inakaribia.
Eneo hilo liko kusini zaidi ya yale yanayokumbwa mara nyingi na vimbunga kila mwaka nchini Philippines.
No comments:
Post a Comment