Sunday, May 27, 2012

POLISI WASUBIRI MTUHUMIWA ATOE HAJA


Polisi nchini Canada wanasema bado wanamsubiri mtuhumiwa mmoja aliyeiba na kumeza kipande cha almasi, aende haja kubwa ili waweze kupata ushahidi.
Mtandao wa habari wa Stuff.co.nz umesema mtuhumiwa huyo anadaiwa kumeza kipande cha almasi chenye thamani ya dola elfi ishirini wiki iliyopita. Bwana huyo Richard Mackenzie Matthews anadaiwa kuingia katika duka la sonara mjini Ontario na kuiba na kumeza kipande hicho cha almasi.
Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi na wapelelezi wamekuwa wakisubiri almasi hiyo yenye uzani wa karati 1.7 itoke kwa njia za asili kutoka tumboni mwake. Sajini wa polisi Brett Corey amesema mtuhumiwa huyo amekwenda chooni mara kadhaa lakini almasi hiyo imegoma kabisa kutoka.
Katika siku za mwanzo mtuhumiwa huyo alikuwa akipewa chakula laini laini, lakini hatua hiyo haikufanikiwa, na hivi sasa bwana huyo anapewa chakula anachotaka yeye. Bado wanasubiri.

No comments:

Post a Comment