Tuesday, May 29, 2012

KOCHA GHANA ATANGAZA KIKOSI

Asamoah Gyana na Dede Ayew wote nje


Mshambulizi matata Asamoah Gyan hayuko kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kilichotajwa na Kocha Kwesi Appia.

Wengine waliotemwa ni mwamba wa Chelsea Michael Essien na Andre 'Dede' Ayew ambaye ana jeraha.Gyan ameachwa nje hata baada ya shinikizo kwamba ajumuishwe kwenye kikosi cha Ghana.
John Paintsil na aliyekuwa nahodha wa Ghana John Mensah nao pia hawamo.
katiuka kikosi chake kipya kocha Appiah amewajumuisha wachezaji sita wapya wengi wakiwa wanachezea soka la kulipwa ulaya. hata hivyo amejumuisha wachezaji tisa toka ligi ya nyumbani.
Asamoah Gyan aliamua kujiondoa toka timu ya taifa baada ya kushambuliwa na mashabiki baada ya uchezaji wake duni katika michuano ya kombe la bara afrika la hivi majuzi.
ilikuwa inatarajiwa kwamba angelirejea katika timu kabla ya mwezi ya Juni.
kwa upande wa Ayew , alifanyiwa upasuaji hivi majuzi nae Essien alisema atashughulika zaidi na timu yake ya Chelsea.

Kikosi cha Ghana:

Golkipa: Adam Kwarasey (Stromsgodset, Norway), Robert Dabuo (Wa All Stars), Daniel Adjei (Liberty Professionals), Ernest Sowah (Berekum Chelsea)
Walinzi: Samuel Inkoom (Dnipro, Ukraine), Daniel Opare (Standard Liege, Belgium), Harrison Afful (Esperance, Tunisia), Richard Kissi Boateng (Berekum Cheslea), Masawudu Alhassan (Genoa, Italy), John Boye (Rennes, France), Lee Addy (Dalian Aerbin, China), Daniel Addo (Arsenal Kyiv, Ukraine) Rashid Sumaila (Dwarfs), Jerry Akaminko (Manisaspor, Turkey), Isaac Vorsah (Hoffenheim, Germany)
Viungo: Anthony Annan (Vitesse Arnhem, Netherlands), Derek Boateng (Dnipro, Ukraine), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese ,Italy), Rabiu Mohammed (Evian, France) Richard Mpong (Medema) Albert Adomah (Bristol City, England), Christian Atsu (Rio Ave, Portugal), Ishamel Yartey, (Servette, Switzerland), Sulley Muntari (AC Milan, Italy), Kwadwo Asamoah (Udinese, Italy).
Washambulizi: Jordan Ayew (Marseille, France), Dominic Adiyiah (Arsenal Kyiv, Ukraine), Ben Acheampong (Kotoko), Emmanuel Baffour (New Edubiase), Emmanuel Clottey (Berekum Chelsea).
<

No comments:

Post a Comment