Jeshi la Uganda linasema kuwa limemkamata afisa
mwandamizi wa kundi la wapiganaji la LRA - kundi ambalo limekuwa
likiwauwa na kuwateka nyara watu Afrika mashariki na ya kati, kwa zaidi
ya miaka 20.
Jeshi la Uganda linasema limemkamata kamanda mwandamizi wa LRA, Caesar Achellam kando ya Mto Mbou katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Limesema Achellam alikuwa na bunduki tu ya aina ya AK-47 na risasi chache.
Ingawa LRA inasemekana kuwa na wapiganaji mia mbili-tatu tu, hata hivo imeleta maafa nchini Uganda, Sudan Kusini, Congo na Jamhuri ya Afrika ya Kati, kwa kuuwa na kuwatesa watu, pamoja na kuwateka nyara watoto wao na kuchoma moto nyumba zao
No comments:
Post a Comment