Wassira alikumbwa na zahma hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani ya mjini Bunda.
Katika mkutano huo, Wasira aliulizwa maswali matatu na kijana mmoja
aitwaye Joashi Kunaga ambayo baadhi yalionekana kumkasirisha.
Maswali hayo pamoja na kumtaka aeleze ni kwa nini eneo la Shule ya
Msingi Balili limechukuliwa na aliyekuwa mkuu wa wilaya, Chiku Galawa,
ambaye sasa ni mkuu wa mkoa wa Tanga na wananchi walishalalamika lakini
yeye hajawahi kulizungumzia.
Swali la pili kijana huyo alitaka kufahamu ukosefu wa maji katika
Hospital ya DDH Bunda ambako sasa hivi wagonjwa wanalazimika kutoa maji
majumbani mwao huku wakati ziwa liko km 11 toka mjini Bunda.
Katika swali lake la tatu alimuuliza kuwa katika mkutano huo alikuwa
anahutubia kama mbunge, waziri au kada wa CCM kwani alitakiwa kufahamu
kuwa Bunda ina wachama wa vyama vingi.
Baada ya kuulizwa maswali hayo Wassira alisimama katika hali
iliyoonyesha kuwa ana hasira na kuaanza kujibu maswali hayo kwa ukali.
Wassira alianza kujibu swali la kwanza la Kunaga akisema kuwa hawezi
kulisemea hilo ni la watu wa ardhi kwa madai kuwa kama mtu alikuwa na
pesa zake akaomba akapewa yeye hawezi kulizungumzia.
Kuhusu suala la maji alisema kuwa maji yapo katika mchakato na kwamba
wananchi watarajie kupata maji muda si mrefu jibu ambalo wananchi
walilikataa na kudai kuwa ahadi zake kuhusu maji zimekuwa za uongo
tangia mwaka 2007 hadi leo amekuwa akisema uongo.
Akijibu kuhusu hoja ya yeye kuhutubia kama mbunge au waziri, Wassira
alionekana kujawa na hasira na kuuliza kwa ukali, “Kwani Wenje alikuja
kuhutubia hapa hivi karibuni kama nani?”
No comments:
Post a Comment