Friday, May 18, 2012

MECHI YA MWISHO KWA DEL PIERO


Alessandro Del Pierro
Alessandro Del Pierro
Mchezaji mashuhuri wa timu ya Italia na klabu ya Juventus, Alessandro Del Piero anatazamiwa kucheza mechi yake ya mwisho jumapili hii dhidi ya Napoli katika fainali ijulikanayo kama Coppa Italia mbele ya umati wa watu kwenye uwanja wa Stadio Olimpico mjini Rome.
Del Piero mwenye umri wa miaka 37 akiwa ni nahodha wa klabu ya Juventus ni shujaa wa mjini Turin, na katika kipindi chake amefunga mabao 290 katika mechi 704 aliyoshiriki, ingawa bodi ya klabu yake haijamuongezea mkataba na huenda akaelekea Marekani msimu ujao.
Katika kipindi cha miaka 19 ya uchezaji wake, Del Piero ameshinda Ligi ya Serie A mara sita, kombe led Coppa Italia mara moja, Ligi ya mabingwa na kombe la Kimataifa la kombe la Ligi za mabingwa duniani pamoja na Kombe la Dunia la mwaka 2006.
Del  Piero
Alessandro Del Pierro
Mwaka huo huo ambamo aliwoshiriki kombe la dunia mjini Berlin, alikubali kushuka daraja kutoka daraja la Serie A hadi Serie B klabu ya Juventus iliposhushwa daraja kufuatia kashfa ya kupanga matokeo ya mechi.
Wiki iliyopita, aliaga mashabiki wake na Ligi ya Serie A ambapo aliweza kufunga katika mechi ya Juventus dhidi ya Atalanta 3-1 na klabu yakew kujitokeza kua ya tatu kumaliza msimu wa Ligi bila kupoteza.
Del Piero aliondolewa katika kipindi cha pili, akiitikia mwaliko wa kusimama mbele ya uwanja wa Juventus, eneo maarufu la Curva Sud akiwapungia mkono mashabiki waliojaa machozi, kabla ya kuelekea upande wa pili wa uwanja kupokea shangwe za mashabiki.

No comments:

Post a Comment