Sunday, May 20, 2012

KULIKONI NGELEJA?


Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini,William Ngeleja
Frederick Katulanda, Geita
MABANGO yenye lengo la kumsafisha aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja yamebandikwa katika sehemu kadhaa katika Jimbo lake la Sengerema, Mwanza.Habari zilizopatikana jana mchana kutoka Sengerema zinasema mabango hayo yalianza kubandikwa juzi usiku na watu ambao walikuwa wakitumia gari.

Ngeleja ni mmoja wa mawaziri sita walioachwa katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri wiki mbili zilizopita na katika uongozi wake amekuwa akituhumiwa kwa kushindwa kumaliza tatizo la umeme, ufisadi wa fedha za umma katika sekta za nishati na madini.

Mabango yanayomsafisha mbunge huyo ni kivuli (photocopy) cha moja ya kurasa za gazeti linalotoka mara moja kwa wiki, ambalo lilichapisha makala yenye kichwa cha habari kisemacho: ‘Zito Kabwe amsafisha Ngeleja.”

Maudhui ya makala hayo yanamsafisha Ngeleja kwamba hahusiki na kashfa ya ufisadi wa Sh600 bilioni ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambayoo ni moja ya sababu zilizomfanya mbunge huyo kutupwa nje ya Baraza la Mawaziri.

No comments:

Post a Comment