Monday, January 23, 2012

Hali ya kibinadamu yahofia Sudan kusini


Sudan kusin
Wapiganaji wa kikabila Sudan kusini
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa shughuli za misaada ya dharura ya kibinadamu zitaathiriwa vibaya katika nchi ya sudan kusini kutokana na mapigano ya kikabila yaliyofanyika katika wiki za hivi karibuni nchini humo.
Sasa inakadiriwa kuwa zaidi ya watu laki moja na elfu ishirini wanahitaji msaada, idadi hiyo ikiwa ni zaidi ya mara dufu ya wale waliouhitaji awali.
Mfululizo wa mashambulio ya kuvizia ya wafugaji katika jimbo la Jonglei ulisababisha mapigano baina ya makabila ya Lou Nouer and Murle mwezi uliopita.
Watu wengi waliuawa na maelfu ya watu wameyakimbia makazi yao kutokana na mapigano hayo.
Maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan kusini wamekanusha hutuma kuwa walizorota kushughulia suala hilo ipasavyo mapema.
Migogoro ya kikabila ya mara kwa mara imekuwa ikitishia hali ya usalama wa taifa hilo jipya zaidi barani Afrika

No comments:

Post a Comment