Jeshi la Nigeria linasema
limewapiga risasi na kuwauwa wafuasi 11 wa kikundi cha wapiganaji wa
Kiislamu, Boko Haram, kaskazini-mashariki mwa nchi.
Juma lilopita watu kama 185 waliuwawa katika mji mwengine wa kaskazini, Kano, kwenye mashambulio kadha ya mabomu.
Boko Haram ilisema ilifanya mashambulio hayo, na imeonya kuwa itaendelea na ugaidi hadi mfumo wa sharia unafuatwa Nigeria nzima.
No comments:
Post a Comment