Thursday, December 29, 2011

HOT NEWS...WANANCHI KIGAMBONI NUSURU WAUE MTUHUMIWA WA UPIGAJI NONDO

WANANCHI wenye hasira kali wakazi wa Kigamboni kata ya Mwangata katika manispaa ya Iringa nusuru wamuue kwa kichapo kijana mmoja anayetuhumiwa kuwa ni mmoja kati ya watuhumiwa wa upigaji nondo katika eneo hilo.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kuwa ni mmoja kati ya vijana wa jambazi sugu ambalo linaendelea kutafutwa katika eneo hilo Msafiri Ilomo ambaye alipata kukutwa na mali mbali mbali zinazodaiwa kuwa ni mali ya wizi zaidi ya Lori moja katika nyumba yake iliyovunjwa na kuchomwa moto baada ya serikali kuamuli ibomolewe.

Wakielezea juu ya tukio hikio hilo wakati wakizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com wakazi wa eneo hilo akiwemo diwani wao Galus Lugenge walisema kuwa kijana huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kutokana na zoezi linaloendelea la kusaka wahusika wote wa mtandao huo ambao wametajwa na mtuhumiwa huyo kabla ya kupigwa na kupoteza fahamu usiku wa leo.


Hata hivyo walisema kuwa zoezi la kuwasaka wahusika zaidi wa tukio hilo bado linaendeklea na kufanywa na wananchi wa kata hiyo hasa wakazi wa Kigamboni.

No comments:

Post a Comment