Bale alifunga mara mbili wakati Tottenham ilipoilaza Norwich kwa
mabao 2-0 na kuweka rekodi ya ushindi wa nane katika mechi kumi za Ligi
Kuu ya England.
Redknapp amesisitiza ni vilabu tajiri tu duniani ndio vinaweza kumnyakuwa mshambuliaji huyo lakini akaweka sawa Bale hauzwi
"Amejigamba: Ni vilabu kama Barcelona, Man City au Real Madrid ambao wanaubavu wa kulipa gharama za kumsajili."
Redknapp hakusita kuonesha namna anavyomhusudu
Gareth Bale ambaye ana umri wa miaka 22, na hadi sasa ameshapachika
mabao manane msimu huu kwa klabu yake ya Tottenham pia mabao matatu kwa
timu yake ya taifa ya Welsh.
Meneja huyo wa Tottenham ameongeza: "Ni mchezaji wa ajabu sana. Ana kila kitu, sioni udhaifu wowote katika uchezaji wake.
"Anaweza kufunga kwa kichwa, ana nguvu kama dume
la ng'ombe, ana mbio sana, chenga na mikwaju mikali. Na muhimu zaidi ya
yote ni kijana mwerevu."
Bale alijiunga na Tottenham akitokea
Southampton mwaka 2007 kwa kitita cha paundi milioni 7 lakini bei yake
kwa sasa imepanda sana kutokana na kuimarika kwa kiwango chake kwa siku
za hivi karibuni katika Ligi na pia mashindano ya Ulaya.
Mwezi Oktoba mwaka 2010 alipofunga mabao matatu
pekee dhidi ya Inter Milan kwenye michuano ya Ubingwa wa Ulaya, dunia
ilianza kumkodolea macho, lakini Redknapp amebainisha iwapo timu yoyote
ya England au kutoka nje itapigwa chini.
Tottenham ipo nyuma kwa pointi saba dhdi ya
vinara wa ligi Manchester City, huku wakiwa na mechi moja mkononi na
wameipiku Chelsea inayoshikilia nafasi ya nne kwa pointi nne pia wakiwa
na mechi moja mkononi.
No comments:
Post a Comment